RONALDO ACHAMBUA LIGI KUU YA HISPANIA


Winga machachari toka Ureno anayekipiga katika klabu ya soka ya Real Madrid ya nchini Hispania Ameendelea kuonyesha uwezo uliomfanya apate tuzo ya uanasoka bora wa dunia baada ya kufunga mabao matano katika mechi zake nne za ligi kuu ya Hispania.Timu zilizopata kibano toka kwa Cristiano Ronaldo ni Derpotivo La COruna,Xerez,Villareal,Osasuna.

UNITED YAICHAMBUA CITY


Ndoto za Kocha wa klabu ya soka ya Manchester United Sir Alex Ferguson kuona wanawanyamazisha majirani zao Manchester City yalitimia pale walipoweza kuwapa mabao 4-3 huku mshambuliaji wa Kiingereza Michael Owen akipachika bao la ushindi katika dakika ya 96`

MAN CITY YAMNASA ADEBAYOR


Mshambuliaji hatari wa klabu ya soka ya Arsenal,Mtogo Emmanuel Adebayor amesajiliwa katika klabu ya soka ya Manchester City kwa kitita cha paundi milioni 20 kwa muda wa miaka mitano.Kwa hiyo mshambuliaji huyo atajiunga na wachezaji wengine mahiri waliosajiliwa na kocha Mark Hughes ambao ni Roque Santa Cruz,Gareth Barry na Carlos Tevez

OWEN ATUA MANCHESTER UNITED


Klabu ya soka ya soka ya Manchester United ya nchini Uingereza yafanikiwa kumsajili mshambuliaji gwiji wa kiingereza aliyemaliza mkataba wake wa kuichezea Newcastle United,Michael Owen.Mahetani hao wekundu wa Manchester wamemsaini mchezaji huyo kwa mkataba wa miaka miwili ambao utamfanya awe analipwa kitita cha paundi 50000 kwa wiki.

OWEN KWENDA MANCHESTER UNITED


Mshambualiaji mahiri wa Kiingereza aliyemaliza mkataba wake wa kuichezea Newcastle United,MICHAEL OWEN,yupo katika hatua za mwisho kusaini kuichezea klabu bingwa ya nchini Uingereza,MANCHESTER UNITED.Usajili huo unaonekana ni kama kichekesho kwa wadau wengi wa soka ukichukulia majeraha yalimkumba Owen katika misimu mitatu Iliyopita wakati anachezea NEWCASTLE UNITED.

GALACTICOS WA PEREZ WATAFANIKIWA?


Ikiwa ni mwezi mmoja baada ya FC Barcelona kuwa mabingwa wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE,LIGI YA HISPANIA na COPA DEL REY.Wapinzani wao wakuu Real Madrid CF,wameonekana wakitaka kuvunja utawala huo wa Barcelona kuanzia nchini Hispania hadi Barani Ulaya.Real Madrid Wamefanikiwa kuwasajili wachezaji mahiri katika ulimwengu huu wa soka ambao ni Cristiano Ronaldo,Ricardo Izecson Dos Santos Leite "KAKA`",kARIM BENZEMA,RAUL ALBIOL na wengine ambao wanahusishwa na kuhamia klabuni hapo akiwemo mchawi wa winga wa kifaransa anayekipiga katika klabu ya Fc Bayern Munchen,FRANK RIBERY`.Kutokana na usajili huo wa gharama kubwa uliofanywa na Rais wa Real Madrid Florentino Perez,JE UNADHANI REAL MADRID WATAWEZA KUTWAA MAKOMBE YOTE KATIKA MASHINDANO WATAKAYOSHIRIKI?. TOA MAONI YAKO KWA KUTUMA UJUMBE WA MAANDISHI KATIKA SIMU YAKO WENYE NENO "NDIYO" kama watanikiwa au "HAPANA" KAMA UNADHANI HAWATAWEZA KUFANYA HIVYO KWENDA NAMBA +255716239490.

BENZEMA ASAJILIWA BERNABEAU


Klabu ya Real Madrid ya Hispania yamsajili mshambuliaji hatari wa kifaransa aliyejuwa anachezea klabu ya Olympique Lyonnais,Karim Benzema kwa kitita cha paundi milioni 35.Hivyo klabu hiyo yenye maskani yake Santiago Bernabeau imeshasajili nyota wanne hatari duniani ambao ni KAKA`,CRISTANO RONALDO PAMOJA NA RAUL ALBIOL

CRISTIANO RONALDO ATINGA MADRID!!!


Klabu ya Real Madrid ya Uhispania yafanya kufuru kwa kumnyakua winga hatari wa kireno aliyekuwa anakipiga katika klabu ya Manchester United kwa dau lililovunja rekodi ya Dunia ya paundi milioni 80.Mreno huyo amesaini mkataba wa kuichezea Madrid kwa miaka 6 kwa hiyo ataunda safu kali ya ushambuliaji iliyo tayari na mbrazili Ricardo KAKA.

KAKA ASAJILIWA REAL MADRID


Klabu ya soka ya Real Madrid ya nchini Hispania yamsajili kiungo wa kibrazili wa AC MILAN ,Ricardo Izecson Dos Santos Leite,kwa kiasi cha paundi milioni 59.Mbrazili huyo ameingia mkataba wa miaka 5 kuitumikia klabu hiyo yenye masksni yake Santiago Bernabeau.

KAKA ABAKI AC MILAN


Kiungo hatari wa Ac Milan ,Ricardo Kaka` ameamua kubaki na klabu yake na kuikacha klabu ya Manchester City inayomilikiwa na waarabu wa Dubai Group of Company

SIMBA YAIWAZA YANGA

Klabu ya Simba imekumbwa na mchecheto wa mpambano kati yao na watani wa jadi YANGA itakayopigwa Oktoba 26.Katibu mkuu wa simba,Mwina Kaduguda amesema hawali wala hawanywi wakijiandaa na mpambano huo wa kukata na shoka dhidi ya watani wao wa jadi,Yanga ,utakaofanyika katika uwanja wa taifa ,jijini Dar es salaam
Karibu kwenye blogspot yangu ,itakayokupa habari mbalimbali za soka kutoka ulaya, historia za timu na wachezaji na mambo mbalimbali ya majuu

CHELSEA YAANDAA PAUNI MILIONI 100 KWA AJILI YA KAKA`

KLABU YA SOKA YA CHELSEA IMEANDAA KITITA CHA PAUNDI MILIONI 100 KWA AJILI YA KUMNASA MSHAMBULIAJI WA KLABU YA SOKA YA CHELSEA HABARI HIYO NI KWA MUJIBU WA GAZETI LA The Sun